Habari
Ufaransa yawa nchi ya kwanza duniani kupiga marufuku vikombe na sahani zinazotupwa baada ya kutumika (disposable)
Ufaransa imekuwa nchi ya kwanza duniani kupiga marufuku matumizi ya vikombe na sahani zinazotupwa baada ya kutumika (disposable).
Sheria mpya ya Ufaransa inataka asilimia 50 ya vyombo hivyo vitengenezwe kwa malighafi ambazo zinaweza kuoza nyumbani, hadi kufikia January 2020.
Namba hiyo itapanda hadi kufika 60% ifikapo January 2025.
Vikombe 150 visivyorudiwa kutumiwa, hutupwa kila sekunde nchini humo sawa na vikombe bilioni 4.73 kwa mwaka.
Uamuzi huo umepongezwa na wengi.