Habari

Uganda kuanza majaribio ya chanjo ya Covid-19

Uganda inatarajiwa kuanza kufanyia binadamu majaribio ya chanjo ya Covid-19 mwezi Novemba, Ripoti ya gazeti la Daily Monitor imewanukuu maafisa wa Wizara ya Afya.

Chanjo hiyo imeandaliwa kupitia ushirikiano kati ya Taasisi ya utafiti ya Uganda na Chuo Kikuu cha Uingereza.

Mkuu wa Jopokazi linalohusika na majanga Monica Musenero, amenukuliwa akisema awamu ya kwanza ya majaribio ya chanjo hiyo itahusisha Waganda 10.

Awamu ya kwanza ikifanikiwa, awamu ya pili itajumuisha watu kati ya 100 hadi 200 ikifuatiwa na awamu ya mwisho itakayojumuisha watu kati ya 1,000 na 3,000,alisema.

Sehemu kubwa ya mradi huo umegharamiwa na Chuo Kikuu cha Uingereza .

Taifa hilo la Afrika Mashariki kufikia sasa imethibitisha kuwa watuzaidi ya 7,000 walioambukizwa virusi vya corona huku 75 wakifariki.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents