UGANDA: Wanafunzi wa chuo kikuu waandamana na kuvamia kituo cha polisi – Video
UGANDA: Wanafunzi wa chuo kikuu waandamana na kuvamia kituo cha polisi - Video
Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda wamevamia kituo cha polisi, kudai kuachiliwa huru kwa wenzao 15 waliokamatwa walipokuwa wakiandamana dhidi ya kuongezeka kwa karo ya masomo iliyoidhinishwa mwaka jana.
Wanafunzi 15 walikamatwa siku ya Jumatatu walipokuwa wakijaribu kuandamana kuelekea katika ofisi ya rais Yoweri Museveni kumuomba aingilie kati mzozo huo , limeripoti gazeti la Daily Monitor.
Picha zilizotumwa kwenye mtandao wa Twitter zinaonyesha wanafunzi hao wakikamatwa nje ya lango la Chuo kikuu na wanajeshi pamoja na polisi.
15 arrested as Makerere students protest tuition increment #MonitorUpdates via Damali Mukhaye pic.twitter.com/9A3bB2zoKV
— Daily Monitor (@DailyMonitor) October 22, 2019
Walichukuliwa katika kituo cha polisi cha Wandegeya huku wakisubiri upelelezi ufanyike, limesema gazeti hilo.Wanafunzi wenzao walivamia kituo cha polisi Jumanne kudai waachiliwe huru.
Makerere University students storm Wandegeya police station demanding for the release of their colleagues arrested earlier for protesting tuition increment https://t.co/PGq3yT8mfD #MonitorUpdates by Alex Esagala pic.twitter.com/djvZ6loAIQ
— Daily Monitor (@DailyMonitor) October 22, 2019
Traffic at Wandegeya traffic junction paralysed as Makerere students protest 15% cumulative fees increment https://t.co/PGq3yT8mfD #MonitorUpdates via ALEX ESAGALA pic.twitter.com/pD6Cd9PJNn
— Daily Monitor (@DailyMonitor) October 22, 2019
Ongezeko la 15% liliidhinishwa na baraza la Vyuo viku nchini Uganda. Wanafunzi wanatakiwa kuanza kulipa ada yenye ongezeko hilo kwa miaka mitano ijayo baadaye kila mwanafunzi atatakiwa kulipa 75% zaidi.
Mchambuzi wa masuala ya kiuchumi na kijamii nchini Uganda Akol Amazima anasema ”Wasimamizi wa vyuo vikuu wanapaswa kutafuta njia za kuhakikisha kwamba wanapata pesa za kuendesha shule ili kupunguza maandamano kama hayo”
Unaweza pia kusikiliza: