Uingereza yaungana na Ufaransa, Ubelgiji nusu fainali kombe la dunia
Timu ya taifa ya Uingereza imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la dunia baada ya kuifunga Sweden kwa jumla ya mabao 2 – 0.
Mabao ya Uingereza yakifungwa na Maguire dakika ya 30, kisha Dele Alli akaja kuhitimisha karamu ya magoli dakika ya 58 na kuwafanya the three lions kutinga hatua ya nusu fainali na kuungana na Ufaransa pamoja na Ubelgiji.
Harry Kane ni mchezaji wa nne kuifungia Uingereza goli hatua ya mtoano ya michuano ya kombe la dunia, baada ya kufanya hivyo Alan Mullery, David Platt na Rio Ferdinand.
Vikosi vya pande zote mbili Sweden: Olsen, Krafth, Lindelof, Granqvist, Augustinsson, Larsson, Ekdal, Forsberg, Claesson, Berg, Toivonen. Kwa upande wa Uingereza: Pickford, Walker, Stones, Maguire, Trippier, Lingard, Henderson, Alli, Young, Sterling, Kane.