Habari

Ujasiri wa wakulima wa bangi wamshangaza DC

Mkuu wa Wilaya ya Nzega, mkoani Tabora, Godfrey Ngupula ameshangazwa na ujasiri walionao wananchi wanaolima mashamba makubwa ya bangi kwa kujiamini kama hakuna serikali.

Akizungumza na wanahabari wakati akiwa kwenye operesheni ya kukamata na kuteketeza bangi,alisema baadhi ya wananchi wamegeuza hifadhi ya Igombe iliyopo mpakani mwa wilaya za Nzega kugeuzwa kuwa mashamba ya bangi.

“Sijawahi kuona watu wanalima bangi kwa kujiamini kiasi hiki tena kwa wingi kama hakuna Serikali, tutahakikisha bangi yote inateketezwa na watuhumiwa wote kufikishwa mahakamani,” alisema Ngupula

Aidha Mkuu wa Polisi Wilaya ya Nzega, Costantine Mbogambi alisema jeshi hilo litapiga kambi msituni kuhakikisha mashamba yote yanateketezwa.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents