Burudani

Ujerumani kujenga bomba ‘refu’ la kusafirisha bia

Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni!! Wakati nchi yetu ya Tanzania ikiingia mkataba na Uganda kwa ujenzi wa Bomba la kusafirisha mafuta kutoka mjini Hoima hadi Tanga hii tofauti kabisa na ujerumani ambapo hao wapo mbioni kujenga bomba la kusafirishia pombe kama hujui basi acha nikung’ate sikio.

Heavy metal fans will be able to guzzle endless pints of beer at at Wacken Open Air festival thanks to a four-mile pipeline that will pump 400,000 litres of the booze to the venue

Waandaaji wa Tamasha moja maarufu la muziki wa rock lijulikanalo kama Wacken Open Air Festival nchini Ujerumani wamewahakikishia wateja wao laki moja (100,000) kwamba, kamwe msimu huu mpya hawatokumbwa na uhaba wa pombe kwani watajenga bomba refu la kusafirisha kinywaji hicho maeneo yote kutakakofanyika tamasha hilo.

The underground pipeline will serve 100,000 rock fans at the festival in Schleswig-Holstein, northern Germany

Taarifa kutoka mtandao wa Metal Insider zinasema mbomba hilo litakuwa na urefu wa Kilometa 7 na upana wa nchi 14, huku likitarajiwa kutoa lita 6 za pombe kwa sekunde moja.

The beer pipeline is already in the works and is expected to be ready just in time for the concert which runs from August 3 to August 5

Maamuzi ya kujenga bomba hilo la pombe yamekuja baada ya malalamiko kutoka kwa wahudhuriaji wa tamasha hilo wakidai kila mwaka limekuwa likishindwa kuwahudumia vinywaji vya kutosha kitu ambacho kinasababisha bei ya vinywaji kuongezeka maradufu.

Beer trucks will drive straight from the brewery to the festival site to help service the massive demand for booze. They will park on the side of the street, connect to the pipeline and start pumping in chilled beers

Ujenzi wa bomba hilo utagharimu kiasi cha Euro milioni 1 sawa na shilingi bilioni 2.5 za kitanzania huku likitarajiwa kukamilika mwezi July siku chache kabla ya Tamasha hilo kuanza.

It will allow bar staff to pour six pints in just six seconds at the world's biggest heavy metal festival, which will be headlined by Marilyn Manson and Status Quo

Ujerumani inakadiliwa kuwa ni nchi ya 3 kwa utumiaji wa pombe duniani ambapo kila mwaka mwananchi mmoja hutumia lita 115.5 za pombe ikiwa nyuma ya nchi za Ireland na Jamhuri ya Czech.

Wacken beer pipeline

Tamasha la Wacken Open Air festival ni moja ya matasha makubwa ya muziki wa Rock duniani ambapo mwaka huu litafanyika Tarehe 3-5 ya mwezi Augosti kwenye viunga vya mji wa Schleswig-Holstein kaskazini mwa Ujerumani na baadhi ya wasanii watakaotumbuiza ni wakongwe Marilyn Manson na Status Quo.

By Godfrey Mgallah

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents