Habari

Ujue mji ghali zaidi duniani, upo Africa

Mji mkuu wa Angola, Luanda, umechukua nafasi ya kwanza kama mji ghali zaidi duniani, huku mji wa Hong Kong ukishika nafasi ya pili.

Mji mkuu wa Angola, Luanda

Takwimu hizi zimetolewa na shirika la Mercer ambalo lilifanya utafiti. Katika takwimu hizo miji ya Tokyo, Zurich na Singapore pia nayo inachukua nafasi tano za kwanza. Mji wa London ulishuka hadi nafasi ya 30 hasa kutokana na kushuka kwa thamani ya paundi.

Utafiti huo wa kila mwaka huangazia masuala kadha kando na gharama ya kukodi nyumba. Utafiti huo huangazia gharama ya vitu 200 kwa kila mji, ikiwemo nyumba, usafiri, mavazi, chakula na burudani.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents