Wema Sepetu

Ujumbe wa Wema baada ya gazeti la Filamu kuandika ‘Wema kunyongwa China…Ishu ya dawa za kulevya’

‘Wema kunyongwa China’ ndio kichwa cha habari iliyomtoa machozi Miss Tanzania (2006) Wema Abraham Sepetu leo iliyoandikwa na gazeti liitwalo ‘Filamu’ katika ukurasa wake wa mbele.

_DSC1055 copy

Wema ambaye ni CEO wa kampuni ya Endless Fame leo alianza kwa kupost picha ya gazeti hilo na kuandika “Hahahahha.. haya niombeeni watanzania…. aisee… magazeti ni noumerrr… mambo ya kunyongwa tena na wakati sufuria zina shake zenyewe… dah… this made my day”

wema filamu

Na masaa mawili baadaye hiki ndicho Wema alikiandika kupitia Intagram kuhusiana na kilichoandikwa na gazeti hilo.

“Dah, Siwezi sema niko happy, im not at all, na sikuwahi kufikiria kwamba magazeti yetu ipo siku yatakuwa na gut ya kuandika uongo wa namna hii. Just because nakaaga kimya ndo muone kwamba mnaweza nionea all da time, roho inaniuma sana, naumia kwasababu nimechoka kuchafuliwa jina bila sababu.

Nimesema nitoke zangu kimya kimya kuja huku kujihangaikia zangu kuhusu kazi zangu ila nimeonekana nimekuja kuuza unga na nitanyongwa soon. Wen are you guys gon leave me in peace..sidhani kama nishawahi kumkosea mtu yeyote kati yenu. Maskini ya Mungu naishi maisha yangu mwenyewe sina habari na mtu. Sijawahi hata kufikiria kufanya those stuff. Nimeumia sana. Da last time I cried was wen nilipoambiwa nina pepo la ngono…leo ninalia ten aim jus so so hurt… God help me please.”

Wema siku za karibuni amekuwa aki post picha mbalimbali zinazoashiria yuko nje ya nchi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents