HabariUncategorized

‘Ukiacha msosi, kitu muhimu kwangu kuliko vyote duniani ni mitandao ya kijamii’ – afunguka kijana Msomi

Kama ulikuwa hujui, basi taarifa hii njema ikufikie kwa wewe mtumiaji wa Vodacom kwani kwa sasa unaweza kununua programu za simu (Apps) kutoka katika duka la Google Play Store bila kutumia akaunti yako ya Benki.

Teknolojia hiyo imekuja baada ya mtandao wa simu za mkononi wa Vodacom Tanzania kuzindua huduma ya kulipia kwa njia ya vocha (muda wa maongezi) ambapo watumiaji wao watanunua kwa kulipia kwa salio la kawaida.

Huduma hii ya Vodacom imemfanya Mwanafunzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari cha DSJ, Raymond Casto kudai kuwa amefurahishwa zaidi na huduma hii kwani inamfanya aweze kufanya kazi zake kwa urahisi.

Raymond amesema kuwa yeye siku zote ukitoa kula jambo lingineĀ  ambalo hawezi kuacha kwa siku ni kutumia mitandao ya kijamii, sana sana pale anapokuwa anatumia mtandao wa Vodacom kufanya manunuzi ya Apps anazozipenda kwa kutumia njia yenye usalama zaidi.

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents