Habari
UN: Lazima tusitishe utengenezwaji wa silaha za nyuklia
Umoja wa Mataifa, Ijumaa itatekeleza mkataba wa kupiga marufuku silaha za nyuklia.
Mkataba wa Kuzuia Kuenea kwa Silaha za Nyuklia unajumuisha ahadi ya kuacha kufanya utafiti, majaribio pamoja na utumiaji wa silaha hizo ambazo ni tishio.
Mataifa yenye silaha za nyuklia hayakutia saini mkataba huo.
Lakini wanaharakati wana imani kuwa hatua hiyo inaongeza shinikizo la kuachana na silaha za nyuklia na katibu wa umoja wa mataifa anaelezea hatua hiyo kama muhimu katika kufikia lengo la kusitisha utengenezaji wa silaha za nyuklia