Burudani
Unafiki ni kirusi kinachoua sanaa yetu – Mboto
Mchekeshaji maarufu, Mboto amewachana baadhi ya wasanii wenye tabia ya kuwachukia wenzao.
Akiongea na gazeti la Mtanzania, Mboto alisema, “Ukweli ni kwamba wasanii wengi ni wanafiki ndiyo maana wanavuma kidogo na kupotea.”
“Lakini kama uko kiroho safi huwezi kupotea kwenye tasnia. Hiki ni kirusi hatari sana kinachoua sanaa yetu ya filamu. Wasanii tupendane, tuache team zisizo na maana,” aliongeza.