Burudani
Unataka kumshirikisha Alikiba? Fikiria upya
Alikiba ametangaza kuacha kufanya vitu viwili vikubwa kwenye muziki wake – kupiga playback na kufanya collabo!
Hivi karibu muimbaji huyo alisema kuanzia sasa atakuwa akifanya muziki wa live peke yake na sasa amesema amesitisha kushirikishwa na wasanii wengine.
Akiongea na 255 ya XXL kupitia Clouds FM jana, Alikiba amesimama kufanya collabo kwakuwa yupo busy akirekodi album zake mbili. Hata hivyo amesema pamoja na kuendelea kurekodi, tayari kibindoni anazo album nne zilizokamilika.