Michezo
US Open: Mashabiki wamtupia lawama Drake baada ya Serena kuondolewa kwenye nusu fainali
Mashabiki wanamlaumu Drake baada ya girlfriend wake Serena Williams kushindwa kwenye nusu fainali ya mashindano ya US Open.
Drake alikuwa uwanjani kumshangilia Serena aliyekuwa akijaribu kuwa mwanamke wa kwanza mweusi tangu Steffi Graf mwaka 1988 kushinda mataji manne ya grand slam kwenye kalenda ya mwaka.
Ni mchezaji wa Italia, Roberta Vinci aliyeizima ndoto hiyo.
Kutokana na kushindwa kwa Serena mashabiki wake walihisi Drake ndiye aliyekuwa na mkosi kuwepo uwanjani hapo na wameanzisha hashtag, #BlameDrake.