Michezo

USAJILI: Morata wa Madrid atua rasmi Chelsea

Mshambuliaji Alvaro Morata amefanikiwa kusaini mkataba rasmi wa kujiunga na Chelsea.

Morata ambaye ametokea Real Madrid ya Hispania amesaini mkataba wa kujiunga na mabingwa hao wa ligi kuu ya Uingereza kwa msimu uliopita kwa mkataba wa miaka mitano.

Hata hivyo dau la uhamisho wa mshambuliaji huyo limekuwa na utata ndani yake huku gazeti la Telegraph likidai mchezaji huyo amesajiliwa kwa paundi milioni 80 huku vyombo vingine vikidai amesajiliwa kwa paundi milioni 70.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents