Burudani

Usanii wamfanya kayumba afiche makucha yake

Msanii Kayumba kutoka Mkubwa na Wanawe ambaye pia ni mshindi wa shindano la BSS 2015, amefunguka sababu zinazomfanya asitumie jina lake vibaya.

Fid Q amewahi kurap kwenye wimbo wake ‘Agosti 13’ kuwa “Ustaa ni mzigo wa mwiba, ukiubeba utaumia.” Kupitia kipindi cha Zero Planet cha Ice FM ya Njombe, muimbaji huyo amesema msanii ni kioo cha jamii na kila kitu ukifanya jambo baya heshima yako inapungua.

“Msanii ni kioo, kwa hiyo mimi nikifanya jambo la ajabu linaweza kunishusha. Kwa hiyo heshima pia inapungua, so msanii ni heshima na msanii ni kioo. Msanii ni kila kitu,” ameongeza kuweka mkazo katika tofauti ya watu hao wawili.

Kayumba kwa sasa ameachia ngoma mpya aliyomshirikisha Aslay inaitwa ‘Mtoto Mbichi’.

Na Gami Dee
Instagram: @gamideetz
Email: [email protected]

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents