Usiku wa Khanga za Kale
Mbunifu mkongwe kutoka Faibak Fashion Asia Idaruos Hamsini amezungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa atafanya onyesho liendalo kwa jina la ’Usiku Kanga za kale 2010’.
Asia alisema kuwa onyesho hilo litafanyika siku ya Ijumaa tarehe moja October katika Ukumbi wa Diamond Jubilee ikiwa na lengo la kukuza hadhi ya kanga , na kwasababu kanga ni moja ya vazi la Mtanzania.
Awali Asia aliongezea kuwa kutakuwepo na burudani kutoka Morden Taarabu ,Khadija Kopa,Rukia Ramadhani,Sabah Mchacho,na Baby Madaha kutoka BSS watakaotumbuiza na pia wabunifu wa mavazi na mastaa mbalimbali watapanda jukwaani kuonyesha mavazi ya kanga.
Onyesho hilo limedhaminiwa na Tusker Lager , Michuzi Blog,Big Solution, Antelope Tours, Clouds FM,Mlimani Television,Valye Spring,Mryard,Channel Ten,Habari Co-operation,TBC1, Full shangwe, Abaya Center, Gema Sound, I-View photography, Eventlights,pamoja na Shear illusion.