Usiyoyajua kuhusu AIRTEL
MWANZO nilikuwa sijui kwa nini AIRTEL wanasema HAMIA AIRTEL, ndipo nikaona bora nikatembelee kwenye banda la mtandao huo na kujipatia elimu kutoka kwa mawakala ambao wapo wakitoa kuhudumia hiyo kwa wateja, nilichokipata hapo niliamini sasa ni lazima watu WAHAMIE AIRTEL, kwa sababu zifuatazo….
KWANZA AIRTEL wanatoza kiasi kidogo cha fedha, yaani NUSU SHILINGI kuanzia saa 12 asubuhi mpaka saa tano usiku bila mchecheto, na kama haitoshi wanakupunguzia zaidi mpaka robo shilingi kuanzia saa tano za usiku mpaka saa 12 za asubuhi bila ya hata longolongo wala ubabaishaji, huku wakikutoza NUSU BEI hapa wanamaana yaani wao wanachukua shiling 3 ‘tu’ kupiga mtandao wowote hapa nchini.
Ili kukuonyesha AIRTEL sio wababaishaji katika mitandao, wanakupa muda wa bulee kwa kutumia muda wa hewani, kusalimu ndugu jamaa na marafiki zako kwa kupitia huduma ya Me2u , kisha wanakupa nyongeza ya asilimia 10, kila unapoongeza salio kupitia huduma ya AIRTEL RUSHA hapo kwa hapo.
Bado AIRTEL wanakuunganisha na midundo ya muziki wa kisasa na ile uipendayo kupitia AIRTEL FLEVA, utakuwa unapata Fleva kalikali popote ulipo na kwa wakati wowote na kukufanya ujisikie huru. Sio wewe ‘tu’ hata wale wanaokupigia pia unaweza kuwapatia burudani kwa kubonyeza namba 15578, na kuwafanya wasiboleke wakati wakikusubili upokee simu.
AIRTEL wakazidi kunishawishi mimi na wengine ambao tulikuwepo kwenye mabanda yao yanayotoa huduma kwa wateja, kutokana na hii huduma ya AIRTEL MONEY, ambayo unauwezo wa kutumana kutumiwa fedha popote ulipo na kwa muda wowote. Zaidi na zaidi wanakupa uwezo wa kuibeba benki yako kiganjani, kwa kuhamisha akaunti yako ya fedha kutoka benki na mpaka kiganjani kwenye simu yako.
Katika huduma hiyo ya AIRTEL MONEY, wanakuwezesha kulipia usajili wa vyuo mbalimbali ‘HELBS’, na kama unaona haitoshi unaweza kulipia Ankala ya Maji, bili ya umeme, chuo Marekani, na Dstv kwa raha zako, bila kupata usumbufu wowote.
pia wanakuwezesha kufanya mawasiliano mazuri tu, na Kilimo kwanza hasa katika zao la Tumbaku kwa kukupatia taarifa isiyo na shaka hata kidogo kutoka AMIS Tobacco, kupiga namba ya AIRTEL *154*45 na kumalizia na alama ya reli.
Zaidi ya hapo AIRTEL wamekuja na funga mwaka kwa kukupa nafasi ya kulala maskini na kuamka tajiri kwa kushiriki Shindano la KWANJUKA na kutuma meseji kwenda namba 15656 na kujishindia kitita cha fedha kuanzia milioni, 10, 5 au 1 ni kwa mwezi wiki na siku. hapo sasa nikaamini kuna ulazima wa kila mmoja KUHAMIA AIRTEL, maana inajua watu wanachokihitaji kwa karne hii.
Pia AIRTEL wamekuwa wakitoa zawadi ya papo kwa hapo, katika mjengo wao wa Sabasaba katika mashindano madogo na makubwa waliyokuwa wakichezesha hapo, kwani unaweza kujiondokea na Kapelo, T-shert, plastiki ya maji na mazagazaga mengine.
Mpaka naondoka hapo nikaridhika na KUHAMIA AIRTEL, nakushauri na wewe uhamie AIRTEL wewe ndugu na jamaa zako…………….. By Mo