Habari
Utafiti: Mama wa nyumbani wana furaha zaidi kuliko wanaofanya kazi
Utafiti uliofanywa nchini Uingereza umebaini kuwa akina mama wanaokaa nyumbani huonekana kuona maisha kuwa na thamani zaidi kuliko wale wanaoenda kazini.
Wanawake hao huepukana na hisia za kuboreka, kuchanganyikiwa ama hisia za kutojiona hawana thamani.
Utafiti huo ulibaini pia kuwa watu waliooa/olewa wameridhika zaidi kuliko wale wanaoishi pamoja bila kufunga ndoa na wana furaha zaidi kuliko wale walio single ama waliotarakiana.
Utafiti huo ulitokana na survey iliyofanywa kwa watu takriban 165,000 walioulizwa namna walivyoridhika, wanavyohisi uthamani, furaha ama wasiwasi katika maisha yao.