Bongo Movie

Uwoya yupo ‘serious’ kuhusu mipango ya ndoa na Jaguar

Irene Uwoya amesema ingawa Jaguar alishindwa kuja kuzungumza na wazazi wake kuhusu ndoa yao, bado wanawasiliana vizuri na kila kitu kipo sawa.

10895131_873265689390899_1051658226_n

Akizungumza na Bongo5 leo, Irene amesema mahusiano yake na Jaguar yapo japo hajafanya maamuzi ya kuolewa.

“Jaguar hakuja kuna vitu ambavyo vilitokea vikasababisha asije,” amesema mrembo huyo. “Kila siku naongea naye na uamuzi wake upo pale pale. Mimi mwenyewe bado sijafanya maamuzi ya kusema niolewe lakini akija ndo tutaongea kila kitu.”

Haya hivyo Irene amesema hawezi kuzungumzia ndoa yake na mcheza soka wa Rwanda, Ndikumana waliyezaa naye mtoto mmoja aitwaye Krish.

“Sasa kuhusu hilo nisingependa kuliongelea, mimi nadhani sijui hata nisemeje, sipendi kuongelea mambo yangu binafsi.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents