Uzuri wa mafuta ya nazi katika ngozi ya binadamu
Mafuta ya nazi yasiyo na kemikali na hutumika kwa wakubwa na hata watoto. Harufu yake huwa ile ya asili zaidi kuliko mafuta yanayotengeneza kwa madawa, ambayo yanayoweza kuleta madhara katika ngozi ya mwanadamu.
Fahamu faida ya mafuta ya nazi katika ngozi:
a. Mafuta ya nazi hung’arisha ngozi
Siyo sehemu za ndani tu ya mwili zinazofaidika na mafuta ya nazi, kama unataka kuwa na ngozi nzuri yenye mng’aro na yenye afya na muonekano wa asili basi paka mafuta ya nazi kila siku kwenye ngozi yako, mafuta ya nazi yana uwezo mkubwa katika kuua bakteria, virusi, na vijidudu vya aina yeyote vinavyoweza kuidhuru ngozi.
b. Huzuia maradhi mengi hatari mwilini
Kama ilivyo katika kuipunguza kolesteroli, mafuta ya nazi yanao uwezo mkubwa katika kuzuia na kutibu magonjwa mengine sababu ya kuwa na kiasi kingi cha asidi iitwayo lauric acid.
Utafiti mwingi umeendelea kuthibitisha kuwa hii lauric asidi hubadilishwa kuwa asidi mafuta nyingine ijulikanayo kwa kitaalamu kama ‘monolaurin’ ambayo inayo sifa ya kudhibit na kuvizuia baadhi ya virusi ikiwemo vile vya ukimwi kuziingia na kuzidhuru seli za mwili na kusababisha maradhi mwilini. Ili kutibu virusi vya ukimwi inashauriwa kunywa glasi 4 za tui la nazi kila siku kwa muda wa miezi mitatu mpaka minne na utaona maajabu.
c. Hutumika kulainisha uke mkavu
Kuna wanawake wana tatizo la kuwa na uke mkavu muda wote hata wakisisimuliwa vipi bado huwa wakavu, kuondokana na tatizo hilo pakaa mafuta ya nazi katika uke wako na utaona faida yake tena bila madhara yeyote hasi.
Kumbuka:
Unaweza kutengeneza mafuta hayo nyumbani kwako na ukaepuka kutumia mafuta yenye kemikali, mafuta haya ni mazuri kwa watu wote.
Chanzo: Fadhil Paulo
Na Laila Sued