Michezo
Van Gaal arejesha furaha Man United
Manchester United wamefanikiwa kuchukua kombe ikiwa ni kombe la kwanza kwa kocha Louis Van Gaal la mashindano ya kimataifa ya Guinness nchini Marekani. Manchester United ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya mahasimu wao wakubwa, Liverpool katika mchezo wa fainali uliomalizika usiku wa jana mjini Miami, Marekani.
Darren Fletcher na Rooney wakiwa wameinua Kombe la Kimataifa
Wafungaji wa mabao hayo, Rooney dakika ya 55, Mata 57 na Lingard 88, baada ya Gerrard kutangulia kuwafungia Liverpool kwa penalti dakika ya 14.