Van Gaal: Mbinu yetu ya uchezaji imeanza kufua dafu
Kocha wa klabu ya Manchester United Louis Van Gaal amesisitiza kuwa mbinu yake ya uchezaji katika timu yake umeanza kufua dafu,huku timu hiyo ikiwa inaendelea kushindana katika makombe matatu.
United ambayo ipo katika nafasi ya sita iko pointi tatu nyuma ya nafasi ya kushiriki katika kombe la vilabu bingwa.
United itaiyalika Liverpool katika uwanja wa Old Trafford siku ya Alhamisi ,huku United ikijaribu kubadilisha matokeo ya 2-0 ili kuweza kufuzu kwa robo fainali ya michuano hiyo ya Europa.
”Nadhani mbinu hiyo inafanya kazi ,alisema Van Gaal,akikana madai kwamba klabu hiyo imefali katika uongozi wake.Hatupati matokeo mazuri sana.Sio mazuri sana ukifikiria kwamba ni lazima uwe bingwa wa ligi,ushinde kombe la Europa ama upate ushindi wa kombe la FA.Kuna wenzetu wengi ambao hawapiganii makombe matatu”.