Burudani

Vanessa Mdee atishia kuliamsha ‘dude’

Umemiss kusikia ngoma mpya kutoka kwa Vanessa Mdee? Basi kaa mkao wa kula.

Ni takriban miezi sita imepita tangu mrembo huyo wa Bongo Flava alipoachia wimbo wake ‘Cash Madame’, kipindi chote hiko ameonekana kuwa kimya kwenye kuachia nyimbo zake na badala yake ameonekana akishirikishwa kwenye kazi nyingi mfuluizo zilizotoka hivi karibuni.

Vanessa kupitia mtandao wa Instagram, amewashtua mashabiki wake kwa kuwaweka tayari kuwa muda sio mrefu anakuja kuliamsha dude kwa kuachia ngoma yake mpya.

“We are what we repeatedly do. Excellence, then, is not an act, but a habit. ?
See you now Kigali IJN, all Gods people say Amen. ?? Alafu NALIAMSHA DUDEEEE ANYTIME ?? #SheKing,” ameandika Vee katika mtandao huo.

Muimbaji huyo ameshafanya kazi kadhaa ambazo zipo tayari ikiwemo aliyoshoot video na Navio wa Uganda mwezi uliopita.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents