Habari

Venezuela kujiondoa kwenye umoja wa OAS

Nchi ya Venezuela imetangaza kujiondoa katika shirika la umoja wa mataifa ya Marekani Kusini (OAS ) kwa madai kuwa, nchi zilizopo ndani ya jumuiya hiyo zinaingilia masuala ya ndani ya nchi yao.

Akiongea na kituo cha runinga cha taifa (VTV), Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo, Delcy Rodriguez amesema, “Katika OAS, tulitangaza kwamba hatua hizi za usumbufu, zimeegemea upande mmoja, haramu.Tutachukua hatua za haraka za kuandaa barua kwa OAS na kuelezea ni ya kujiondoa kwa Venezuela kwenye huu umoja.”

“Kesho, kama alivyotaka Rais Nicolas Maduro, tutawasilisha barua ya kujiondoa katika umoja wa OAS na tutaanza hatua hizo ambazo zitachukua miezi 24,” ameongeza.

Watu wapatao 30 wamefariki dunia katika maandamano yanayoendelea nchini humo kwa takribani wiki ya tatu sasa,wakimtaka rais Nicolas Maduro kujiuzulu kutokana kuzorota kwa uchumi wa nchi hiyo jambo lililosababisha upungufu mkubwa wa chakula.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents