Michezo
Venus Williams atupwa nje nusu fainali US Open
Mchezaji tenis raia wa Marekani, Sloane Stephens ametinga hatua ya fainali ya mashindano ya wazi ya Marekani ‘US Open’ baada ya kumshinda,Venus Williams katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.
Mchezaji tenis raia wa Marekani, Sloane Stephens(kulia), na Venus Williams(kushoto)
Stephens mwenye umri wa miaka 24 amefanikiwa kumtoa Williams kwa jumla ya seti 6-1 0-6 7-5 na hivyo kuungana na Madison Keys ambaye naye ametinga hatua hiyo kwa ushindi wa seti 6-1 6-2 dhidi ya CoCo Vandeweghe.
Mchezaji tenis Madison Keys
Marekani yaingiza wanawake wanne nusu fainali US Open
Ikiwa ni kwa mara ya kwanza kwa Marekani kuingiza wanawake wanne katika hatua ya nusu fainali ya michuano mikubwa tangu walivyofanya hivyo mwaka 1985.