Burudani

Video: Aloneym ataja sababu za muziki wa Zanzibar kutotusua

Mtayarishaji wa muziki kutoka kisiwani Zanzibar, Aloneym amedai kuwa ukosefu wa menejimenti na  usimamizi nzuri  kumpelekea kuleta ugumu  katika tasnia hiyo.

Aloneym amieleza Bongo5, kuwa muziki wa  Zanzibar unaonekana mgumu kutokana na kukosa uongozi mzuri na usimamizi hafifu ndio unaofanya kuonekana kuwa hakuna wanamuziki wengi na kupelekea muziki huo kuwa mgumu kwa baadhi ya wasanii.

“Kweli Zanzibar, muziki ni mgumu na ugumu unasababishwa labda na strong management hatuna, so we need strong menegement labda muziki watu watauona. Kwa sababu hatujapata watu wenye misukumo wanaotakiwa na ndiyo maana tunaonekana tunakuwa chini daily,” amesea Aloneym.

Pia ameongeza “Wasanii wanaoonekana wanafanya vizuri ni kwa sababu wana strong management, ukimwangalia AT ni mtu ambaye ana management yake, Bell  Black na wengine ndiyo maana wanakuwa wanafanya vizuri.”

Na Laila Sued na Salum Kaorata

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents