Michezo
Video: Asha Baraka ashinda kwa kishindo uchaguzi wa Simba, awafunika wote Mwina Kaduguda haamini
Mmiliki wa bendi ya Twanga Pepeta na mwanachama wa klabu ya Simba Mama Asha Ramadhan Baraka maarufu kama Asha Bara amefanikiwa kushinda kwa kishindo kwenye nafasi ya ujumbe ya timu hiyo kwakupata kura nyingi kuliko Mwina Kaduguda na wagombea wengine wote wanafasi hiyo katika uchaguzi mkuu uliyofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere uliyopo Posta jijini Dar es Salaam.
Katika matokeo ya uchaguzi huo Asha Baraka amefanikiwa kupata jumla ya kura 1187 na kuwazidi wajumbe wote akiwemo Mwina Kaduguda aliyepata kura 577.