Burudani

Video: Baada ya Alikiba na Diamond, Erick Omondi aibuka na Michael Jackson

Mchekeshaji kutoka nchini Kenya, Erick Omondi ameendelea kuonyesha uwezo wake kwa kile anachokifanya kila siku kuhakikisha mashabiki wake wanazidi kufurahi.

Erick Omondi kwa sasa ameachia video ya wimbo wake mpya ‘Be the Highlander’ ambao amefanya remix ya ngoma ya Michael Jackson inayokwenda kwa jina la You Rock My World.

Huu umekuwa ni utaratibu wa kawaida kwa mchekeshaji huyo, utakumbuka hivi karibuni alitoa refix ya ngoma ya Alikiba ‘Seduce Me’ ambayo aliipa jina la Shock Me, pia aliwahi kufanya remix ya ngoma ‘Aje’ kutoka kwa muimbaji huyo.

Kama hiyo haitoshi aliweza kufanya tena remix ya ngoma ‘Zilipendwa’ kutoka WCB na kuipa jina la Zilitemwa, bila kusaha ile ya Diamond ‘Eneka’ ambayo aliita Taga.

Itazame hapa Original version ya You Rock My World kutoka kwa Michael Jackson.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents