Burudani
Video: Baada ya kutohudhuria BET kisa ujauzito, Card B aelezea ushindi wake
Rapper wa kike kutoka nchini Marekani, Card B amewashukuru mashabiki wake na kila mmoja kufuatia ushindi alioupata kwenye tuzo za BET 2018.
Tuzo hizo ambazo zilitolewa usiku wa kuamkia leo June 25, 2018 Los Angles nchini Marekani, Card B alishindwa kuhudhuria kutokana na ujauzito alionao kwa sasa.
Jambo hilo lenye kheri katika maisha yake halikumzuia kushinda tuzo ya Best Female Hip Hop Artist Award, Pia ameshinda katika kipengele cha Best Collaboration Award kupitia ngoma yake ‘Bartier Cardi’ aliyomshirikisha 21 Savage. Hata hivyo Card B ameeleza kuwa wanawame wanaofanya muziki wa Hip Hop hawapewi support kama inavyotakiwa.