Michezo
Video: Beckham afurahishwa na surprise ya mwanae kwenye birthday yake
Jumatano hii ya Mei 2 ilikuwa ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwa mkongwe wa soka wa Uingereza, David Beckham, lakini kubwa zaidi lililomfurahisha ni surprise aliyoipata kutoka kwa mwanae Brooklyn.
Beckham alikuwa akipata chakula cha mchana na familia yake kwenye moja ya migahawa nchini Uingereza lakini alishangaa kumuona mtoto wake huyo akitinga maeneo hayo katika kipindi ambacho alitakiwa kuwa chuoni mjini New York, Marekani.
Hilo lilimfurahisha sana Beckhs mpaka kushindwa kuzuia hisia zake na kuandika kwenye mtando wa Instagram, “The biggest surprise of the day…. Welcome home @brooklynbeckham X happy birthday @davidbeckham I love u so much x kisses.”