Burudani

Video : Dj Khaled aachia dude jipya na Rihanna

Ikiwa imesalia wiki moja kuipata albamu yake ya kumi ‘Grateful’, Dj Khaled leo rasmi ameachia ngoma yake mpya ya “Wild Thoughts,” itakayopatikana katika albamu hiyo.

Wimbo huo uliokuwa ukipigiwa promo ya kutosha na Dj Khaled katika mitandao ya kijamii na kuandika maneno yanayoashiria kuwa na shahuku ya kupata sauti ya Rihanna, ameuachia rasmi leo na mwanadada huyo amesikika na kuonekanana katika ngoma hiyo.

Pia wimbo huo msanii msanii aitwaye Bryson Tiller naye ameweza kusikika na kuonekana. Albamu ya Grateful inatarajiwa kutoka rasmi wiki ijayo (Juni 23) huku ikiwa na ngoma kaliz zipatazo 23 na ameshirikisha wakali wa muziki kama Jay Z, Beyonce, Alcia Keys, Nas, Travis Scott, Rihanna, Niki Minaj, Chance The Rapper na wengine.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents