Burudani

Video: Jay Moe anawatamani wasanii hawa ndani ya lebo yake

Msanii wa muziki wa hip hop Bongo, Jay Moe ambaye kwa sasa anatamba na ngoma ‘Nisaidie Kushare’ ameonyesha yupo tayari kuanza kuwasaini wasanii watakao kuwa china ya lebo yake ‘So Famous Entertainment’.


Jay Moe na Climax Bibo wakitoa burudani katika tamasha ya ‘Heshima ya Bongo Fleva.

Jay ameiambia Bongo5 kuwa ameamua kuja na lebo hiyo kwanza kusimamia kazi zake pia ameona kuna vipaji vingi sana mtaani na vinafanya vizuri.

”Bado tunaendelea kupata maombi mengi kutoka kwa wasanii ila kuna wasanii nawapenda kama Mirror, mtu kama Climax, Deddy ambaye nimefanya naye ‘Hili Game’, Damian Soul ni moja ya watu wanaofanya muziki vizuri kabisa. Naona nikiwa na enough money nita invest zaidi” amesema Jay Moe wakati wa show yake siku ya Jumamosi.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents