Burudani
Video: Kayumba afunguka tetesi za kuibiwa fedha za BSS na Mkubwa Fella
Msanii wa Bongo Flava, Kayumba amekanusha fedha alizoshinda katika shindano la BSS kuchukuliwa na Mkubwa Fella.
“Nimepewa fedha zangu taslimu na mimi mwenyewe ndio nilimwambia anijengee nyumba, kila kitu nilikuwa naendesha mimi mwenyewe siyo kwamba yeye amepewa hela anipe mimi, hapana. Yule ni mtu ambaye amenisaidia kabla sijaenda BSS huwa inaniuma sana nikisikia hivyo” Kayumba ameiambia Bongo5.