Habari
VIDEO: Kuanzia sasa bei ya korosho ni tsh 3,300/= kwa kilo, msiponunua tutazila wenyewe – Rais Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo Novemba 12 ametangaza bei mpya elekezi ya korosho ambapo amesema kuwa itanunuliwa kwa Tsh 3,300/= kwa kilo.
Rais Magufuli ameyasema hayo Ikulu Jijini Dar Es Salaam ambapo ameyakataa makampuni 13 yaliyojitokeza kununua Korosho, kwa madai kuwa nayo huenda yakaleta longo longo mwishoni.