Videos
Video: Rais Magufuli aaigiza trafiki aliyetukanwa na mke waziri akiwa kazini apandishwe cheo
Askari wa usalama barabarani aliyeambuliwa matusi ya kumwaga kutoka kwa mke wa mmoja wa mawaziri nchini wakati akitekeleza majukumu yake amekula shavu.
https://www.youtube.com/watch?v=2yFSE1baMKM
Ni kwasababu Rais Dkt John Pombe Magufuli amemuagiza kamanda wa polisi, IGP Ernest Mangu kumpandisha cheo mara moja.
Ametoa agizo hilo wakati akifungua kikao cha Makamanda wa Polisi wa Mikoa. Pia Magufuli amedai kuwa amemuonya waziri huyo pamoja na mke wake.
“Huyo trafiki anajua kazi, na huyo waziri na mke wake nimeshamuambia,” alisema.