Habari
Video: Mazishi ya Ivan yafanya kufuru Uganda
Ivan Ssemwanga ambaye alifariki wiki iliyopita alizikwa jana jioni kijijini kwao Nakalilo katika wilaya ya Kayunga nchini Uganda, lakini msiba huo ulionekana kuvunja rekodi kutokana na waliokuwa watu wa karibu wa marehemu kufanya vitu vilivyowashangaza wengi.
Msiba huo ulihudhuriwa na watu kibao wakiwemo mastaa wa Uganda Jose Chameleone, Bobi Wine, Weasel Manizo na wengine.
Jose Chameleone akiwa katika msiba wa Ivan
Lakini kubwa zaidi linalozungumziwa katika mazishi hayo ni kipindi ambacho watu ambao walionekana kuvalia nguo nyeusi walimwaga pombe, fedha katika kaburi la marehemu Ivan kitendo ambacho hakijazoeleka kikawaida.
Tazama video hiyo hapa chini.
https://youtu.be/nNtSSzHPZjY