Habari

Video: Mfahamu mtu anayecheka saa 24

Belachew Girma ni raia wa Ethiopia ambaye amekuwa maarufu mno kwenye vyombo mbalimbali vya habari duniani kutokana na rekodi yake ya kuwa mtu mwenye uwezo wa kucheka saa 24 kuliko mwingine yeyote yule.

Kwenye mazungumzo yake na BBC, Girma amesema kuwa watu hupenda kuona sura zenye tabasamu na kuamini kuwa kucheka ninjia moja wapo inayomfanya mtu kuondokana na maumivu ya mwili.

”Habara zenu, jina langu ni Belachew Girma natokea Ethiopia. Kila mmoja kati yetu angependa kuona sura ya tabasamu,” amesema Girma.

Belachew Girma ambaye huwa na desturi ya kutembelea makundi mbalimbali vijana, wazee na watoto wadogo kuwapatia furaha ameongeza ”Mimi ni mchekaji namba moja katika rekodi ya dunia, utafiti umethibitisha kuwa unapocheka hupunguza maumivu ya asili mwilini.”

”Hivyo nilianza kufanya mazoezi ya kucheka ili niweze kuishi maisha marefu zaidi na yenye afya, kama tutatengeneza kila mahala wachekaji itakuwa ni kama lugha ya kawaida ya kuwasaliana.”

Belachew Girma anaimani kuwa kupitia kucheka dunia itabaki kuwa salama kwakuwa wachekaji sikuzote hupenda uwepo wa amani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents