Habari

Video: Mfungwa mtukutu duniani aliyetoroka na helkopta gerezani anaswa tena

Baada ya kuchukua miezi mitatu toka kutoroka kwake gerezani hatimae Polisi nchini Ufaransa leo siku ya Jumatano wamefanikiwa kumkamata jambazi sugu, Redoine Faid sambamba na kaka zake wawili huko kusini mwa jiji la Paris.

Chanzo kimoja cha karibu kimethibitisha, Faid ambaye anatokea kwenye kundi la watukutu zaidi nchini Ufaransa lijulikanalo kama ‘notorious ganster’ kuwa amekamatwa.

From stealing sweets to daring prison breaks: The story of France's infamous gangster Redoine Faid

Jambazi sugu, Redoine Faid

Redoine Faid mwenye umri wa miaka 46 amewahi kutoroka jela kupitia helkopta, kijana huyo mtukutu Julai 1 mwaka huu amewahi kutoroka mbele ya jeshi zito kwakutumia mabomu yanayotoa moshi na kufanikiwa kuvunja dirisha la jela.

Video ikionyesha helkopta aliyotumia kutorokea gerezani

Alitoroka jela alipokuwa anatumikia kifungo chake, baada ya watu wenye silaha nzito kuvamia jela hiyo iliyoko Kaskazini mwa jiji la Paris. Watu hao walimchukua na kuondoka naye kwa kutumia helkopta ambayo walikuwa wameiteka.

Police launch manhunt for notorious French gangster after brazen helicopter jailbreak

Hata hivyo nimarakadhaa kwa Mr Faid kufanya mchezo wake wa kutoroka jela mbele ya ulinzi mkali ambapo mapema leo polisi wamethibitisha pia kukamatwa kwake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents