Habari
Video mpya ya Stamina yapata msukosuko
Mkali wa muziki wa Hip Hop kutoka Morogoro, Stamina baada ya jana kuachia video ya wimbo wake mpya ‘Love Me’ aliomshirikisha Maua Sama, leo hii aliripoti kuwa akauti yake ya YouTube kuibiwa lakini baada ya saa moja ilirejea hewani.
Stamina kupitia Instagram ameandika ‘Daah!, Bongo bwana miyayusho sana, tukijitahidi hata kwa juhudi zetu kutafuta ugali wetu kwa kutumia jasho letu na vipaji vyetu bado watu hawaoni. Wamehack account yangu ya YouTube aisee!! nisipate viewers wengi? au ili nisisonge mbele kimziki??? too sad ila sitokata tamaa mpaka mwisho wa uhai wangu, mashabiki zangu samahani kwa usumbufu tatizo linashughulikiwa nitawajulisha wataalamu wakimaliza kulisolve,” aliandika Stamina kabla haijarejea. By Peter Akaro