Burudani
Video: Mtangazaji wa Kenya, Maina, asema wasanii TZ mfano wa kuigwa EA
Mtangazaji maarufu wa Classic 105 ya nchini Kenya, Maina Kageni amefunguka kwa kusema kuwa wasanii wote wa Tanzania wanapaswa kupewa tuzo kutokana na muziki mzuri wanaoufanya Afrika Masharik, Afrika na duniani. Maina ameiambia Bongo5 kuwa mara nyingi akikutana na wasanii wa Kenya na Uganda, huwa anawaambia namna ya kufanya muziki mzuri kama ambao wanafanya wasanii wa Tanzania.