Bongo Movie

Video: Mtoto wa Waziri zamani kuachia filamu aliyooteshwa, afanya audition kuchagua waigizaji 15

Mtoto wa Waziri wa zamani Stephen Wasira, Lilian Wasira, ameamua kuingia kwenye tasnia ya filamu na kueleza sababu zilizomfanya aingie huko na kuanza kuelezea filamu yake ya kwanza atakayoanza kuiandaa wiki ijayo ambayo alioteshwa ndotoni.

Lakini pia Lilian ambaye kitaluma ni Mwanasheria, Jumanne hii kwenye ukumbi wa hoteli ya Green Light iliyopo Tabata, amefanya audition ya kuchagua vijana 15 ambao watashiriki kwenye filamu hiyo inayokwenda kwa jina la ‘Saa Imetimia’.

Majaji katika audition hiyo alikuwa Shamsa Ford, Grace Mapunda na msanii wa muziki wa injili maarufu kama Mapinduzi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents