Burudani
VIDEO: Mwana FA atinga BASATA kuwaombea msamaha Diamond na Rayvanny ‘wimbo mzuri, wawaondolee adhabu’
Rapper Mwana FA ametinga BASATA na kama Mjumbe wa Bodi ya Baraza hilo, kuomba adhabu iliyotolewa kwa Diamond na Rayvanny ya kufungiwa wimbo wao wa Mwanza aidha ifutwe au ipunguzwe.
Akiongea na Waandishi wa Habari mapema leo Novemba 14, 2018, Mwana FA amesema wimbo wa Mwanza ni mzuri kusikiliza kwa kijana aliyevuka miaka 18 hivyo BASATA wangeangalia namna ya kufuta adhabu hiyo.