Habari
Video: Mzee Kilomoni aongoza dua ya kumuombea Mo Dewji
Mmoja wa viongozi wa bodi ya wazamini wa klabu ya Simba Mzee Hamisi Kilomoni hii leo amefanya dua nyumbani kwake kumuombea kwa Mungu Mdhamini Mkuu wa timu hiyo Mfanyabiashara Mohammed Dewji ili kupata wepesi katika matatizo yaliyomkuta.
Familia ya ‘MO’ yatangaza zawadi ya Sh Bilioni moja kwa atakayetoa taarifa zitakazosaidia kupatikana kwa Mo Dewji
Inafahamika kuwa Mo Dewji ambaye ni mfanyabiashara hapa nchini ametekwa na watu wa siyo julikana majira ya saa 11: 35 mpaka saa 11: 40 tarehe 11 Oktoba 2018 Colosseum Hotel Mtaa wa Haile Selasie Oysterbay Dar es salaam kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa familia ambayo imetangaza zawadi ya Sh Bilioni moja mbele ya waandishi wa habari kwa yoyote atakayetoa taarifa zitakazowezesha kupatika kwake.