Michezo
Video: Naifahamu Yanga SC, Simba SC na Azam FC – Kavazovic
Kocha mkuu wa klabu ya Townshp Rollers, Nikola Kavazovic amesema kuwa amekuwa akiwafuatilia kwa ukaribu wapinzani wake wa michuano ya kombe la klabu bingwa barani Afrika, Yanga SC hasa katika michezo yake miwili ya hivi karibuni ya nyumbani na ugenini.
Nafahamu mpira wa Afrika ulivyo na naifahamu, Yanga SC, Simba SC, Azam FC na baadhi ya timu hizi zinachipukia.
Nafahamu kila kitu kuhusu Yanga SC nimekuwa nikiwafuatilia hasa wiki iliyopita kwa michezo yake miwili ya nyumbani na ugenini hivyo najua kila nilichopaswa kujua.