Burudani
Video: Rayvanny atua BASATA baada ya wimbo wa ‘Mwanza’ kufungiwa
Msanii wa muziki Rayvanny amefika kwenye ofisi za Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) baada ya kufungiwa kwa wimbo ‘Mwanza’ kwa madai wimbo huo hauendani na maadili ya Kitanzania.
BASATA ilitangaza kuufungia wimbo huo wa Rayvanny ambao kamshirikisha DiamondPlatnumz unaofahamika kwa jina la Mwanza kwa maelezo kuwa unahamasisha masuala yasiyokubalika katika jamii.