Habari
Video: RC Makonda amtwisha mzigo wa migogoro ya ardhi Waziri Lukuvi ‘Nimefika pahala nimegota’
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda hii leo amezungumza na wakazi wa Wilaya ya Kinondoni katika viwanja vya Bunju akiwa sambamba na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi juu ya kutatua kero na changamoto zinazowakabili juu ya ardhi. Mbele ya Waziri, Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi hao kutumia nafasi hiyo kueleza kero zao zote kwakuwa yeye ndiye mwenyemamlaka hayo nakuwataka kutomhoji tena maswala ya migogoro ya ardhi kwakuwa amewaletea dawa yake.