Burudani

VIDEO: Rihanna ni mama kijacho?, Wadau mitandaoni wauliza ‘Drake alikwama wapi?’

Hatimaye ndoto ya Rihanna aliyowahi kuielezea mbele ya Media kuwa anahitaji kuwa na mtoto kwasasa, Huenda ndoto hiyo imetimia kwani mrembo huyo anaonekana kwasasa ni mjamzito.

Rihanna

Rihanna ambaye usiku wa kuamkia leo alitumbuiza kwenye jukwaa la tamasha la hisani la Diamond Ball 2019 lililofanyika jijini New York-Marekani, Alionekana akiwa na kitumbo huku mashabiki wake wakishangilia na wengine kutaka kumshika.

Hata hivyo, Baada ya kushuka jukwaani na kupita kwenye zulia jekundu, Rihanna aliziba kitumbo chake kwa mikono miwili kukwepa picha za mapaparazi.

Rihanna was spotted clutching her stomach on the red carpet at the 5th Annual Diamond Ball.

Akiwa kwenye Red Carpet alihojiwa na Essence, Ambapo aliulizwa “Mwanamke amekufunza nini kwenye maisha yako?”.

Rihanna alijibu “Mimi ni mwanamke mweusi, Nimezaliwa na mwanamke mweusi, Ambaye na yeye alizaliwa na mwanamke mweusi na hata mimi pia nitazaa mwanamke mweusi.“.

Hii sio mara ya kwanza Rihanna kuonekana na hali kama hii na kuzushiwa kuwa anaujauzito. Kwani hata mwaka 2017 alipatwa na tetesi kama hizo.

Kufuatia video na picha za Rihanna kusambaa mitandaoni, Wadau wengi wamehoji Drake alikosea wapi? mpaka Rihanna anakuja kupata ujauzito na mwaarabu.

Kwasasa Rihanna yupo kwenye mahusiano na mchumba wake wa kiarabu kutoka Saudi Arabia, Bilionea Hassan Jamal.

https://www.instagram.com/p/B2WqrhCAtjQ/

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents