Video: Serikali haikandamizi Wanawake – Mhe. Mabula
Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula amesema Serikali haikandamizi wala haibagui mwanamke kuweza kupata Hati miliki.
Amezungumza Bungeni mjini Dodoma, Naibu Mabula wakati akijibu swali la Mbunge wa Kawe, Halima Mdee lililohoji:
Asilimia kubwa au asilimia zaidi ya 70 ya nguvu kazi ya kilimo ni wanawake lakini ni kwa bahati mbaya sana inapokuja swala la umiliki wa ardhi wanaomiliki ardhi ni pungufu hata ya asilimia 20 na hata ninapozungumza Hati za kawaida na hati za kimila haziwanufaishi wanawake kwasababu sheria za nchi yetu zinatambua sheria za kimila zina ubaguzi, sasa nilitaka Wizara inisaidie katika mpango wenu mpana ya kuweza kufanya maboresho kwenye sekta ya ardhi mna mkakati gani wakuweza kuondoka na Sheria Kandamizi ili umilikiwa ardhi usiwe na ubaguzi hivyo shughuli za uchumi zinufaishe Makundi yote?
Video:Tazama majibu ya Serikali:
Na Emmy Mwaipopo