Video: Serikali kuweka sheria ya kudhibiti matumizi ya shisha
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, amesema serikali ina mpango mkakati wa kutengeneza utaratibu wa kudhibiti utumiaji, uuzwaji na usafirishwaji ya shisha nchini Tanzania ili kuweza kuokoa afya za Watanzania walio wengi.
Mwigulu Nchemba ameyazungumza hayo leo Bungeni mjini Dodoma wakati akijibu hoja mbalimbali za Wabunge.
“Ni kweli serikali mara baada ya kuona kuwa matumizi ya shisha yanaleta athari kubwa kwa afya za binadamu kutokana na utafiti uliofanywa na wizara ya Afya serikali ina mpango mkakati wa kutengeneza utaratibu wa kudhibiti na kutungia sheria kupiga marufuku, utumiaji na uuzwaji na usafirishwaji nchini Tanzania ili kuweza kuokoa afya za Watanzania waliowengi ambao ni nguvu kazi ya Taifa letu,” alisema Mwigulu
Video: Tazama Mjadala kuhusu Shisha
Na Emmy Mwaipopo