Michezo
Video: Sportpesa yaja na kampeni ya kujishindia Bajaj ‘Shinda zaidi na Sportpesa’
Kampuni ya kubashiri michezo nchini ya Sportpesa leo imezindua rasmi promosheni ya kuinua maisha kiuchumi SHINDA ZAIDI NA SPORTPESA itakayo dumu kwa siku 100 ambapo mshindi ataweza kujishindia BAJAJ RE mpya, pesa taslimu au vyote kwa pamoja. Promosheni ya SHINDA ZAIDI NA SPORTPESA inaanza leo Alhamisi 20 Septemba 2018.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa promosheni hiyo leo jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa SportPesa, Tarimba Abbas amesema kuwa hii ni mara ya pili kwa kampuni hiyo kuendesha promosheni kama hiyo kwa wateja wake.